Friday 6 April 2018

JINSI YA KUUZA NA KUTENGENEZA BRAND YAKO KWA KUTUMIA MITANDAO YA KIJAMII


Zama zimebadilika, mambo yamebadilika. Ujio wa intaneti umefanya mapinduzi makubwa katika biashara hasa kwa karne hii ya ishirini na moja. Utangazaji wa biashara kupitia magazeti na televisheni kwa kiasi kikubwa hauna nguvu tena kama ilivyokuwa hapo zamani.

                    



Mitandao ya kijamii imeteka kwa kiasi kikubwa biashara nyingi hii ni kwasababu watu wengi wanatumia mitandao ya kijamii. Na moja wapo ya kanuni za kufanya mauzo ni kuwafata wateja mahali walipo. Wateja wengi wapo kwenye mitandao ya kijamii hivyo ni wajibu wako kuwafata huko.

Wakati watu wengine wanajiunga na mitandao ya kijamii ili waweke picha zao na maandishi ya kuchekesha kusudi wapate like kuna watu wengine wametengeneza pesa kubwa kupitia mitandao ya kijamii. Je wewe umewahi kufikiri kutengeneza pesa kupitia mitandao ya kijamii?

FAIDA ZA KUTUMIA MITANDAO YA KIJAMII
1.    Ni rahisi sana kujifunza hivyo mtu yeyote anaweza kujifunza na kuanza kuitumia mitandao ya kijamii kikamilifu.
2.    Ni gharama ndogo ya kujitangaza kwa wateja ukilinganisha na magazeti na TV.
3.    Mitandao ya kijamii hujenga uaminifu. Watu wanapenda kufanya biashara na mtu wanayemfahamu. Hivyo ni rahisi kupata wateja wanaokufatilia kwenye mitandao yako.
4.    Unaweza kuwasiliana na wateja wako moja kwa moja.
5.    Mitandao ya kijamii itakusaidia kupata wasomaji wa blogu au website yako kama unamiliki blogu au website.
6.    Mitandao ya kijamii itakusaidia kujua na kufanya uchunguzi wa soko. Utajua watu wanataka nini na hawataki nini.
7.    Inakuongezea uthamani. Ukiweza kuwa mtu anayeweka mambo ya maana kwenye mitandao yako, thamani yako itapanda.
8.    Watu watakutafuta na kufanya kazi na wewe. Ukitengeneza jina lako vizuri katika mitandao ya kijamii watu wakubwa watahitaji kufanya kazi na wewe. Mimi ni shuhuda wa hili, baada ya kuanza kuandika Makala mbalimbali katika blogu yangu ya BIDEISM nimekuwa nikitafutwa na watu mbalimbali ili tufanye kazi pamoja.
9.    Itakufungulia connection mpya. Ukiweza kujibrand vizuri utaweza kufanya kazi na kupata connection kubwa ambazo hata kabla ulikuwa huzitarajii.

JINSI YA KUTENGENEZA BRAND YAKO MTANDAONI.
1.    Hakikisha unaandika mambo yanayowagusa watu mara nyingi uwezavyo. Kuna watu wengi wanatafuta namna ya kutatua matatizo yao. Ni jukumu lako kuwaonesha namna gani wanaweza kuyatatua. Hii itakuchukua muda watu kuanza kukuelewa  na muda mfupi ambao utakuchukua ni miezi 6. Watu mara nyingi sio rahisi kukuelewa lakini kadri unavyoendelea watakuelewa. Hivyo usikate tamaa.
2.    Angalia wenzako wanafanya nini katika mitandao yao ya kijamii. Ukiona kuna mtu anafanya kitu ambacho ulikua ukitamani kukifanya mtafute na ikiwezakana omba ushauri kwake akupe njia yeye anawezaje. Kama yeye ameweza unaweza pia. Kama mimi nimeweza, wewe pia unaweza.

3.    Kuwa mtu wa watu. Ukiwajali watu watakujali pia. Unahitaji kuwa mtu wa watu katika mitandao ya kijamii. Wajibu watu kwa heshima, tumia maneno kama; kaka au dada yanasidia sana. Asikwambie mtu watu wanapendwa kuheshimiwa. Ukiwapa heshima watakuja kwako.


4.    Uonesha ujuzi wako:
Kuna watu wengi wana ujuzi lakini kwenye mitandao yao ya kijamii hawoneshi ujuzi huo. Wanafanana na yule mtu aliyepewa talanta akaificha. Usikubali kuwa na ujuzi halafu kwenye mitandao yako ya kijamii hauuoneshi. Ujuzi wako ni pesa uliyoikalia.

JINSI YA KUJITANGAZA KUPITIA MITANDAO YA KIJAMII
Takwimu zifuatazo zinaonesha matumizi ya mitandao ya kijamii nchini Tanzania toka Machi 2017 hadi mwezi Machi 2018:

MTANDAO
ASILIMIA YA WATUMIAJI
Facebook
59.98%
Youtube
17.36%
Pinterest
12.67%
Twitter
5.97%
Instagram
2.27%
Google+
0.67%

Ukichunguza kwa ukaribu unaweza kujua ni mtandao upi ambao una watumiaji wengi. Unahitaji pia kujua wateja wako wanatumia mtandao upi na inakupasa ujiunge pia na mtandao huu. Kumbuka biashara huenda kule wateja waliko. Kama wateja wako wanapatikana WhatsApp hakikisha umejiunga Na WhatsApp pia.

MAMBO YA KUFAHAMU KABLA KUANZA KUTUMIA MITANDAO YA KIJAMII KUJITANGAZA:
·       MALENGO:
Unahitaji kuanza kwa kuandika malengo yako kwanini unataka kutumia mitandao ya kijamii kujibrand na kufanya biashara. Hatupangi kushindwa tunashindwa kupanga, watu wengi hawapangi ndiyo maana malengo yao hayatimii.

·       Jua ni wapi wateja wako. Ukijua watu gani watakua wateja wako utakua umejiweka kwenye wakati mzuri. Je ni vijana? wazee Au wanafunzi, wazazi, kutaja wachache.

·       Ni wapi wanapatikana.
Ukijua ni mitandao gani wateja wako wanapatikana hakikisha unawafata huku. Hapo utakuwa umelishika soko lako.

MAMBO YA KUZINGATIA:
1.    Uaminifu.
Kama hautakuwa mwaminifu katika kazi zako ni bora usifanye biashara kupitia mitandao ya kijamii. Uaminifu ni nguzo kubwa katika kufanya biashara kupitia mitandao.

2.    Kanuni ya 7/1
Kama katika post unazoziweka katika mitandao yako ya kijamii hakikisha post 6 zinazungumzia au kuelezea bidhaa zako na ujuzi wako na post moja ambayo ni ya saba ndiyo iwe tangazo la bidhaa yako. Ukiwa mtu wa kutangaza bidhaa tu utawaboa watu na wataacha kukufatilia. Weka vitu vingi vinavyowaelimisha na ndipo uweke matangazo ya bidhaa zako.

3.    Kuwa muwazi.
Ukionekana kwenye mitandao ya kijamii onekena kama mtaalamu. Usionekane kama watu wengine. Kumbuka watu wanhukumu kava ya kitabu na ni kilicho ndani ya kitabu.
4.    Unahitaji kuwa mbunifu. Usifanye mambo kwa mazoea, kila siku jiulize swali ili: nitafanyaje kwa ubora zaidi ya jana? Hilo ni swali unalopaswa kujiuliza kila siku.

UZUSHI KUHUSU MITANDAO YA KIJAMII
Kuna uzushi mwingi utausikia lakini na kuahakikishia kwamba mitandao ya kijamii ni chaguo jema kama utakua kweli umeamua kijutanua kibiashara.
Uzushi kwamba mitandao ya kijamii ni ya watoto:
Utasikia kuwa mitandao ya kijamii inatumiwa na watoto lakini jambo hilo sio la kweli kabisa. Takwimu zinaonesha kuwa watu wenye umri wa kuanzia miaka 35 ndiyo wamekuwa watumiaji wakubwa wa mtandao wa Facebook, umri kuanzia miaka 24 hadi 34 huongezeka mara mbili kila baada ya miezi sita. Watu wengi wanaotumia mtandao wa Twitter wana umri wa miaka 35-49. Watumiaji wa mtandao wa LinkidIn wanao wastani wa umri wa miaka 41.

Uzushi kuwa unahitaji utaalamu wa teknolojia kutumia mitandao ya kijamii:
Kwenye matumizi ya mitandao ya kijamii hauhitaji kuijua sana teknolojia ndipo uanze kuitumia. Kanuni ya 80/20 inasema 80% ya unachokiweka mtandaoni ni kile unachokitoa na 20% ni ujuzi wa teknolojia. Hivyo usiogope kuhusu teknolojia.

Najua umefunguka sana kuhusu matumizi ya mitandao ya kijamii. Usisoke kusoma Makala zinazofuata kwenye blogu hii. chini kabisa ya blogu hii unaweza kudownload APP ya blogu hii ili upate Makala zinazofuata ili kujifunza Zaidi. Bofya sehemu iliyoandikwa DOWNLOAD OUR APP chini kabisa ya ukurasa huu ili upate APP yetu bure.

Mafanikio Yako Mikononi Mwako.

Ndimi:
EDIUS KATAMUGORA
0764145476

Washirikishe na wenzako Makala hii. Mafanikio ni kitu cha kushirikishana.

Hii ni blogu rasmi ya Edius Katamugora, hapa utajifunza maendeleo binafsi, utapata makala mbalimbali zinazohusu biashara, elimu, hamasa na maisha kwa ujumla. Karibu sana katika blogu hii.

0 comments: