Sunday 12 March 2017

Bustani Zinazoelea (Hanging Gardens of Babylon)

Bustani zinazoelea kwa Nina maarufu la "hanging gardens of Babylon" ni mojawapo kati ya maajabu saba ya dunia. Zilinasadikika kuwa zilikuwa mji wa Babylon ambao leo ni Iraq.

Zilijengwa mwaka 600BC na zilikuwa na urefu wa mita 24.

Aliyezijenga alikuwa ni mfalme Nebuchadnezzar wa pili kwa mke wake aliyeitwa Amytis. Amytis mtoto wa mfalme wa Medes  aliolewa kwa Nebuchadnezzar ili kuleta ushirikiano baina ya pande mbili.

Amyitis alitokea sehemu iliyokuwa na milima na yenye kijani kibichi. Alipoolewa kulikuwa tambarale na hakukuwa na kijani kibichi. Hivyo Nebuchadnezzar aliamua kumtengenezea bustani juu ya jengo ili kumfurahisha mke wake.



Hii ni blogu rasmi ya Edius Katamugora, hapa utajifunza maendeleo binafsi, utapata makala mbalimbali zinazohusu biashara, elimu, hamasa na maisha kwa ujumla. Karibu sana katika blogu hii.

0 comments: