Tuesday 7 March 2017

Umesikia Nini Kuhusu Pesa?


Habari mpendwa msomaji wa Bideism blog. Ni matumaini yangu kwamba umeamka salama na unaendelea kusonga mbele ili kupambana kuelekea mafanikio.
Karibu sana katika mada ya Leo.
Ulipokuwa mdogo na hata muda huu kuna mengi unasikia kuhusu pesa. Wengi wetu tukiwa wadogo wazazi wetu walitwambia maneno kama "mwanangu usipende pesa itakuponza" au hata uko mitaani umesikia maneno kama *matajiri* *ni* *washirikina*, "ukipata pesa uwezi kuwa na furaha hata siku moja. Au wengine tumeambiwa "huwezi kuwa tajiri kwani ukoo wenu nyote ni maskini".
*Bill* *Gates* aliwahi kusema "To be born poor is not your fault, your fault is too die poor" hapa anamaanisha, "kuzaliwa maskini sio kosa lako, kosa lako ni kufa maskini". Ukweli ni kwamba maneno mengi uliyoyasikia toka kwa wazazi,ndugu,jamaa na marafiki au hata huko mitaani ni ya uongo na si ya ukweli hata kidogo.
Watu wengine wanaenda mbali zaidi na kutumia maneno ya biblia kwamba inakataza pesa, utasikia wanasema imeandikwa "Pesa ni chanzo cha maovu yote" hasha!, kwenye biblia hawajaandika ivyo bali imeandikwa '"Kuipenda pesa ni chanzo cha maovu yote" na wala haijaandikwa "Pesa ni chanzo cha maovu yote". Kimsingi ukiweka upendo wako kwenye pesa itakupeleka kweli kwenye kutenda maovu.
√ Mwandishi wa Kitabu cha ACRES OF      DIAMOND anasema "unahitaji kuwa na pesa kwani, pesa ndiyo iliyochapisha biblia,pesa ndiyo iliyowalipa posho wamisionari,pesa ndiyo iliyowasafirisha wamisionari,pesa ndiyo imejenga makanisa" hiyo yote ni kuonesha umuhimu wa pesa.
Kimsingi pesa usaidia kusolve matatizo mengi lakini si yote. Utasikia wanasema "Money talks" wakimaanisha "pesa inaongea", waswahili wanaenda mbali zaidi na kusema "pesa sabuni ya roho". Watu matajiri kwanza ndio wenye kusaidia kutatua matatizo mengi ya watu duniani, angalia watu kama Mark Zukerberg wamerahisisha mawasiliano, Leo hii kuna wasap,Facebook, instagram, kutaja machache. Bill Gates pia amekua mstari wa mbele kupambana na maswala ya malaria barani Afrika na pia amesaidia kuleta maji kwenye nchi zenye ukanda wa maji. Hiyo yote ni pesa inafanya kazi.
√ Badili mitazamo yako hasi kuhusu pesa na anza kupambana kutafuta pesa ili usaidie familia yenu,ndugu na jamii inayokuzunguka kwa ujumla. Kimsingi unatakiwa kuwa tajiri. Jifunze kuwa na matumizi mazuri ya pesa pia itakusaidia.

Definition nzuri ya pesa ni "kitu unachopata baada ya kutoa Huduma Fulani", jiulize Leo utatoa Huduma gani ili upate pesa kutoka kwenye jamii inayokuzunguka.
√ " *See* *you* *at* *the* *top* "
√ By
√ *Edius* *Bide* *Katamugora*
- 0764145476
- 0625951842 (whatsapp)
- Www.Bideism.blogspot.com
Tangazo;
Nimeandika Kitabu kinachoitwa "Barabara ya mafanikio" unaweza weka oda yako mapema. Kwani nakala ni chache.

Hii ni blogu rasmi ya Edius Katamugora, hapa utajifunza maendeleo binafsi, utapata makala mbalimbali zinazohusu biashara, elimu, hamasa na maisha kwa ujumla. Karibu sana katika blogu hii.

0 comments: