Friday 20 April 2018

Kama Ningeacha Chuo Bongo


Mara nyingi nimekuwa nikisikia vijana wengi wakijishauri wao kwa wao na kusema chuo hakisaidii. Mbona matajiri wengi duniani waliacha chuo na wamefanya makubwa duniani.

 Image result for quotes about quitting school

Paul Allen mwanzilishi wa kampuni ya Microsoft hakuhitimu chuo.
Bill Gates mwanzilishi wa Microsoft hakuhitimu chuo. Mark Zuckerberg mwanzilishi wa Facebook hakuhitimu chuo.
T D. Jakes hakuhitimu hata sekondari (highschool).
Joel Osteen hakuhitimu pia elimu ya sekondari.
Said Salim Bakhresa mwanzilishi na mmiliki wa makampuni ya Bakhersa Group aliacha shule ya msingi akiwa na miaka 14.
Na sasa hivi ni watu maarufu na waliofanikiwa sana kiuchumi.

Je kama Mimi ningeacha chuo Leo ningekuwa kama wao?
Unaacha chuo una nini? Hili ni swali ambalo kabla hujaamua kusema unaacha chuo inabidi ukae chini na kujiuliza.

Wakati Bill Gates akiwa na umri wa miaka 16 na Paul Allen akiwa na miaka 19 tayari wakikuwa wamekwisha anzisha Microsoft.
 
Wakati Mark Zuckerberg anaacha kusoma chuo cha Harvard  tayari Facebook ilikua imeanza kufanya kazi.
Je wewe ukitaka kuacha chuo una nini mkononi?
Said Salim Bakhersa katika miaka ya sabini (1970) alikuwa akifanya biashara ya mgahawa huko Zanzibar kwa miongo mitatu mfulilizo. Huko nyuma aliwahi kufanya biashara za mikate, viazi na rambaramba (ice cream)

Wengi wamekuwa wakifikiri kwamba akienda kufanya biashara atatoboa maana amesikia watu wengi wamekuwa matajiri kwa kufanya biashara ili hali hajawahi kuuza hata ubuyu. Maana yangu ni kusema hajui lolote kuhusu biashara lakini amekazana elimu haisaidii.

Elimu haitakusaidia lolote kama utakuwa mtu wa kukaa darasani ukishindana na wenzako ili upate maksi za juu bila kupata ama kuongeza ujuzi. Ili ni tatizo linaloyakumba mataifa mengi hapa duniani katika sekta ya elimu. Watu wengi wanashindania kupata maksi za juu lakini si kupata ujuzi. Kukosa ujuzi ni kukosa maarifa na kama hauna maarifa utaangamia. "Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa." (Hosea 4:6)
 
Ukiwa na mawazo ya kuacha chuo hakikisha una kitu mkononi kitakachokupeleka mahali unakokwenda. Watu unaowaona wamefanikiwa kibiashara walianza zamani mno. "Nilijijenga na kuibuka Tajiri namba moja Afrika mwaka 2008 lakini haikutokea usiku mmoja. Ilinichukua miaka 30 kufikia Leo hii. Vijana wa siku hizi wanatamani kuwa kama mimi lakini wanapenda itokee usiku mmoja, hawafanyi kazi. Kujenga biashara yenye mafanikio inakupasa uanze kidogo na uwe na ndoto kubwa. Safari ya ujasiriamali ni mshikamano wa lengo kuu." alisema Aliko Dangote. Ninaweza kukumbuka wakati nilikuwa shuleni la msingi, ningeenda na kununua makandoni ya masanduku ya pipi na ninaanza kuwauza ili tu kupata pesa. Nilikuwa na nia ya biashara hata wakati huo,” anahitimisha Aliko Dangote.
Ukiwazia kufanya biashara bila kujua yaliyomo ni sawa na kwenda vitani bila silaha. Unategemea nini. Lazima upigwe kipigo kama alichopata Goliathi.

Usiwaze sana kuacha chuo wakati hauna kitu chochote unachokijua. Usiwaze kuacha chuo na kufanya biashara kama haujawahi kufanya biashara ndogo yoyote hata ya kuuza visheti, bangili na heleni.

Walioacha chuo, kuna mambo tayari walikwisha yaweka sawa. Walikwisha iona barabara yao ya mafanikio. Sikushauri uache chuo kama hauna ujuzi wowote na usiwe tu ujuzi bali ujuzi wa kipekee utakaoleta utofauti kwa jamii inayokuzunguka, taifa na hata dunia.

Makala hii ni sehemu ya kitabu cha HOW TO BECOME AN EXPERT WHILE AT SCHOOL. Weka Oda yako kupitia 0758594893.

Mafanikio yako mikononi mwako.

Ndimi: Edius Katamugora
Mwandishi na Mhamasishaji
0758594893
ekatamugora@gmail.com
Www.bideism.blogspot.com

Washirikishe na wengine maana mafanikio ni kitu cha kushirikishana.

Usisahau kupakua APP ya blog hii mwisho kabisa wa ukurasa huu. Bofya sehemu iliyoandikwa DOWNLOAD OUR APP FOR FREE uweze kupata Application yetu.

Hii ni blogu rasmi ya Edius Katamugora, hapa utajifunza maendeleo binafsi, utapata makala mbalimbali zinazohusu biashara, elimu, hamasa na maisha kwa ujumla. Karibu sana katika blogu hii.

0 comments: