Tuesday 24 April 2018

KWANINI UNAHITAJI KUWA NA BLOGU AU TOVUTI YA BIASHARA YAKO




Kila siku nitaendelea kusisitiza jambo hili, ZAMA ZIMEBADILIKA, MAISHA YAMEBADILIKA. Biashara siku hizi zinafanywa kitaalamu Zaidi ya ilivyokuwa zamani.

Siku za nyuma nilizungumzia jinsi mtu anavyoweza kujibranda na kuuza bidhaa zake kupitia mitandao ya kijamii. Kama kuna mtu alianza kufanyia kazi yale niyoyaandika ni matumaini yangu anaona matokeo ya tofauti sasa.

Mbali na kutumia mitandao ya kijamii unahitaji pia kuwa na blogu na tovuti ya biashara yako. Sasa utajiuliza je! Mbona biashara yangu ni ndogo hivyo sihitaji kuwa na blogu au tovuti. Na mimi nitakuuliza, “kwani biashara yako itakuwa hivyo hivyo miaka mitano au kumi ijayo?” kama jibu ni ndiyo basi hauhitaji blogu au tovuti kama jibu lako ni hapana jua kwamba unahitaji kuwa na blogu au tovuti ili kujitanua kibiashara. Katika mitandao ya kijamii kuna watu wengi wa kufatilia lakini mtu akitembelea blogu au tovuti yako anakuwa akikufatila wewe pekee.



Zifuatazo ni faida za kuwa na blogu au tovuti:

1.      Tovuti au blogu yako ni kama benki, yaani inafanya kazi masaa 24. Benki huwa zinafungwa lakini ATM sikuzote hazifungwi zinaendelea kutoa huduma za kifedha. Hivyo hivyo blogu au tovuti yako itakuwa ikitumika masaa ishirini  na nne hata kama haupo kwenye biashara yako  lakini watu wana uwezo wa kuona umeingiza bidhaa gani mpya, bei za bidhaa, n.k.

2.      Tovuti inakusaidia kuwafikia watu walio nje ya mahali ulipo na hata dunia nzima. Blogu yangu ya BIDEISM imekuwa ikisomwa na watu wa mataifa yote. Mtu akiingia google na kutafuta BIDEISM ananipata moja kwa moja.

3.      Blogu au tovuti itakusaidia kutangaza bidhaa au huduma zako. Kupitia blogu na tovuti utawavuta wateja waje kwenye biashara yako kwa njia ya matangazo.

4.      Itakuongezea sifa. Watu wanapenda kufanya kazi au biashara na watu wanaoonekena wataalamu na wale wanaowafahamu na kuwazoea. Mtu akizoea blogu au tovuti yako ni rahisi kufanya kazi na wewe pia ni rahisi kukuamini.

5.      Inatoa sapoti ya kimtandao kwa wateja wako. Kama mtu anashida na biashara yako anaweza kuingia moja kwa moja kwenye tovuti yako au blogu na kupata majibu. Hii itakusaidia pia kuokoa muda wako.

6.      Blogu au tovuti inatoa njia ya watu uwasiliana na wewe. Kwenye blogu yako utaweka jinsi  watu wanavyoweza kuwasiliana na wewe hivyo utawapa mwanya wa kupata mawasiliano yako kiurahisi.

Je unahitaji gharama kubwa kutengeneza blogu?
Unaweza kutengeneza blogu wewe mwenyewe. Njia rahisi ni kutumia mitandao ya Wordpress na Blogger lakini pia unaweza kumwajiri mtu akutengenezee blogu au tovuti yako hii ndiyo njia ambayo nakushauri uifuate kwani utapata kutengenezewa tovuti au blogu nzuri ya biashara yako kutoka kwa wataalamu wa mambo ya kutengeneza blog na tovuti. Kama utahitaji Blogu au Tovuti ya Biashara yako unaweza kuwasiliana nami kupitia namba hapo chini.

"Mafanikio yako mikononi mwako."

Ndimi:
Edius Katamugora
0758594893
ekatamugora@gmail.com

Usisahau kupakua APPLICATION yetu mwisho kabisa wa ukurasa huu sehemu iliyoandikwa DOWNLOAD OUR APP FOR FREE. Bofya hapo utaipata bure.

Mafanikio ni kitu cha kushirikishana washirikishe na wengine.

Hii ni blogu rasmi ya Edius Katamugora, hapa utajifunza maendeleo binafsi, utapata makala mbalimbali zinazohusu biashara, elimu, hamasa na maisha kwa ujumla. Karibu sana katika blogu hii.

0 comments: