Tuesday 1 May 2018

MAMBO 30 NILIYOJIFUNZA MWEZI APRILI

Habari mpendwa msomaji wa BIDEISM BLOG. Ni matumaini yangu kwamba unaendelea vizuri na safari yako ya maisha ya kila siku na bado haujachoka kutafuta maarifa. Kila mwezi tunapaswa kufanya tathimi ya yale tuliyojifunza hivyo nimeona ni vyema nikushirikishe yale niliyojifunza mwezi uliopita unaweza pia upata maarifa yanayoweza kukutoa sehemu moja kuelekea nyingine:

                        

Yafuatayo ni mambo niliyojifunza mwezi Aprili:

1.    Tanguliza upendo kila mahali. Utapata chochote unachokitaka kama utawasaidia kupata kile wanachohitaji
2.    Jifunze kuweka bajeti ya kutafuta maarifa. Kama unavyotenga bajeti ya chakula, tenga bajeti ya kutafuta maarifa.
3.    Ukiona unashindwa mahali jua kwamba unakosa maarifa kuhusu hicho. Ukiumwa kichwa unaenda kwa daktari sababu haujui tatizo la kichwa.
4.    Kitu kigumu ukikipa muda kinakuwa rahisi.
5.    Marafiki unaoambatana nao wana mchango mkubwa katika uchumi wako. Ukichagua wenye fikra za kimaskini jiandae kuwa maskini.
6.    Waache watu wakuchukulie poa usikubali kujichukulia poa. Ukijishushia thamani jua kwamba hakuna atakayekuja kupandisha thamani yako.
7.    Muda pekee wa kutizama nyuma ni pale unapotaka kujua ni hatua kiasi gani umepiga.
8.    Ukitaka kuwa na matumizi mazuri ya muda wako weka vipambele. Fanya mambo ya muhimu.
9.   Mungu hawezi kukupa kitu ambacho bado hauwezi kukifanya. Mungu hawezi kukupa mzigo ambao hauwezi kuubeba.
10.Kile unachokifanya leo ndicho kitakacho tofautisha maisha yako na ya kesho ya baadae maana maisha yako ya kesho yanategemea nini unafanya leo.
11. Unaweza kumaliza wiki bila kutumia mitandao ya kijamii? Kama jibu ni HAPANA jua kwamba umekwisha athirika na matumizi ya mitandao. Kuwa na kiasi katika matumizi ya mitandao ya kijamii.
12.Visingizio na lawama havitakupeleka popote. Acha kulalamika.
13. Kamwe usijilinganishe na mtu mwingine. Kulinganisha kunabagua.
14.Imani ni kama mswaki, utumie kila siku lakini usitumie wa mtu mwingine.
15.Dunia imebadilika zama zimebadilika, kama una biashara hakikisha biashara yako ipo mtandaoni.
16.Fursa zimejificha katika matatizo. Yatizame matatizo kwa jicho la tatu.
17. Umepewa mdomo mmoja na maskio mawili. Jifunze kusikiliza zaidi ya kuongea. Lakini pia jifunze kuwa mtu wa mwisho kuongea.
18.When you update your statuses and apps remember also to update your brain.
19.Muda wa kufuatilia maisha yaw engine umekwisha. Anza kufuatilia maisha yako.
20. Ukiona unaona wivu katika kushangilia maisha yaw engine. Jua kwamba itakuchukua muda kufanikiwa.
21. Tembea na notibuku kila mahali unapokwenda. Fanya hii kuwa tabia yako. Unaweza kupata wazo na usiliandike kisha likapotea. Inawezekana wazo hilo ndilo lingekutoa kimaisha.
22. Jifunze kujitolea katika makampuni makubwa. Huko utapata ujuzi na utaweza KUIBA mbinu mbalimbali za utendaji kazi zitakazo kusaidia katika maisha na kazi zako za baadae.
23. Ukijikuta wewe ndiye mwenye uwezo wa zaidi katika chumba ulichomo. Unahitaji kutafuta chumba kingine.
24.  Kimjaacho mtu ndicho kimtokacho. “Garbage in, Garbage out.” Unachoingiza akilini mwako ndicho unachokitoa.
25.Kuwa mtu wa watu. Dunia ni mji mdogo. Tengeneza marafiki, achana na maadui.
26. Vitu vitatu vya kuweka siri:
a)    Hatua yako inayofuata
b)   Mahusiano yako
c)    Kiwango cha pesa ulichonacho

27.  Fanya kazi nzuri na ioneshe kwa watu. (Hapa tumia intaneti.)
28. Andika kitabu unachotaka kukisoma. Andika unachokipenda na sio kile unachokijua. Andika stori unayoipenda sana, andika stori unayotaka kuisoma. Kanuni hii itumie katika maisha yako na katika kazi yako.
29.  Kama unashawishiwa na mtu Fulani hakikisha unashawishiwa na watu wengine wa namna hiyo katika sekta hiyo. Ukishawishiwa na Mbwana Samatta, watu watasema wewe ni Samatta ajaye, ukishawishiwa na kina Mbwana Samatta wengi, watu watasema wewe ni origino.
30.   Google kila kitu. Namaanisha google ndoto zako, matatizo yako. Usiulize swali kabla ya kuliuliza google. Utapata jibu au utapata swali zuri Zaidi ya lako.

Mafanikio yako mikononi mwako.

Ndimi:
Edius Katamugora
0758594893
ekatamugora@gmail.com

Hii ni blogu rasmi ya Edius Katamugora, hapa utajifunza maendeleo binafsi, utapata makala mbalimbali zinazohusu biashara, elimu, hamasa na maisha kwa ujumla. Karibu sana katika blogu hii.

0 comments: