Monday 5 June 2017

Maneno Matatu Muhimu Kwenye Mahusiano


         
Habari za asubuhi mpendwa msomaji wa BIDEISM BLOG. Ni matumaini yangu kwamba umeamka salama na umejiweka tayari kutimiza majukumu  yako ya leo. Tumshukuru Mungu kwa kutupa siku nzuri kama ya leo. Leo ni siku muhimu, usikubali ipotee. One day can make you grow.

Karibu sana katika Makala ya leo niliyokuandalia.

Wakati anaandika kitabu chake cha NGUZO TATU ZA MAISHA, Mwandishi Lazaro Samwel aliweka mahusiano, kama nguzo mojawapo ya maisha, ukiachana na maendeleo binafsi na ujasiriamali. Ni mwandishi mzuri sana katika tasnia ya uandishi, ukisoma maandiko yake utakubaliana na kile ninachokisema.

Kwenye kitabu hiki, cha Nguzo Tatu Za Maisha, kuhusu mahusiano nimeona maneno matatu muhimu kwenye mahusiano ambayo yatakusaidia kwenye mahusiano yoyote uliyomo, maneno hayo ni:
a)  Asante:
Asante ni neno dogo lenye herufi sita lakini lina maana kubwa sana kwa mtu ambaye uko naye kwenye mahusiano. Neno ili sit u muhimu kwa watu waliokwenye mahusiano au ndoa, ni neno muhimu kwa mtu yeyoyote kwenye jamii. Unapofanyiwa jambo la ukarimu, jifunze kesema asante, mtu aliyekufanyia kitendo hicho ataona unathamini jambo alilolitenda na ataona kwamba unamthamini pia. Ukiletewa zawadi, ukifanyiwa ukarimu, sema “Asante.’’ Jifunze ata kujishukuru mwenyewe, kwa kusema asante, ata pale tu unapoamka kitandani, unapokwenda kuoga, kuna kitu kipya utakiona kama mabadiliko kwenye maisha yako. Neno asante ni dogo lakini wengi linawashinda kutamka. Nakumbuka tukiwa wadogo, mama alikuwa akikuletea zawadi kama vile nguo, usiposema asante, zawadi hiyo ulikuwa ukinyan’ganywa. Ilikua ni njia nzuri ya kutufundisha kushukuru.

b)  Hongera:
Jifunze kumpongeza mwenzako kwa kila jambo zuri analolifanya. Hii itampa motisha kwa kuzidi kusonga mbele kwenye mafanikio na maisha yake kwa ujumla. Hakuna kitu kibaya kama kufanya jambo zuri alafu mtu wako wa karibu hasikupe pongezi, inakatisha tamaa kwa kiasi Fulani. Mtu uliyenaye kwenye mahusiano, akivaa vizuri mwambie “hongera umependeza.” Akifanya vizuri kwenye kitu fulani mwambie “Hongera” hata kama ni jambo dogo.

c)   Samahani
Neno “samahani” ni neno dogo  lakini limesababisha mahusiano mengi kuvunjika na kuishia pabaya kwa watu kushindwa kukiri makosa na kuomba msamaha. Watu wote sio wakamilifu, kukosea kupo tu. Jifunze kusamehe hata kama hujaombwa msamaha. Samehe kila siku kabla ujalala kwani kutunza kinyongo na hasira juu ya mtu ambaye huko naye kwenye mahusiano ni kumkaribisha shetani kuyaingilia mahusiano yenu. Kumbuka mazuri yote ambayo uliwahi kufanyiwa yanazidi kosa moja tu ulilotendewa,\. Jifunze kukiri makosa na kusema “samahani” kwa mtu uliyemkosea hata kama umefanya kosa dogo namna gani. John Billings aliwahi kusema “Hakuna kisasi kilichokamilika kama msamaha.” Kumbe ukitaka kulipiza kisasi kikubwa toa msamaha. Wengine wamekuwa wakiwaza kwamba kuomba msamaha ni kujishusha, lakini hayo ni mawazo mgando (stinking thinking). Jifunze kuomba msamaha kwa kusema “samahani” itakusaidia. “Unforgiveness blocks blessings; forgiveness releases blessings” anasema John Mason mwandishi maarufu wa vitabu vinavyohusu huamasishaji akimaanisha “kutosamehe huondoa Baraka; kusamehe huleta Baraka.”

Nakutakia utekelezaji mwema.

SEE YOU AT THE TOP

Ndimi
Edius bide katamugora
Author and motivational speaker
0764145476/ 0625951842
Email: ekatamugora@gmail.com

Kwa atakaye hitaji kitabu cha Nguzo Tatu Za Maisha anaweza kuwasilaiana nami kupitia namba zilizowekwa hapo juu.

Karibu pia kuweka oda ya kitabu changu kizuri kinachozungumzia mengi kuhusu mafanikio kinachoitwa BARABARA YA MAFANIKIO (Mafanikio yako mikononi mwako).

Washirikishe na wenzako ulichojifunza.

Hii ni blogu rasmi ya Edius Katamugora, hapa utajifunza maendeleo binafsi, utapata makala mbalimbali zinazohusu biashara, elimu, hamasa na maisha kwa ujumla. Karibu sana katika blogu hii.

0 comments: