Friday 28 May 2021

UFAHAMU MTANDAO MPYA WA CLUBHOUSE NA KWANINI UNATAKIWA KUWA HUKO MARA MOJA

 


Miezi miwili iliyopita rafiki yangu Innocent Swai ambaye huwa anaandika katika gazeti la Citizen, (makala zake nyingi huwa zinahusu mambo ya teknolojia) alinipigia simu na katika maongezi yetu alitambulisha kitu kipya. Kitu hicho kipya ulikuwa ni mtandao wa Clubhouse.

Clubhouse ni mtandao ulioanzishwa machi 2020, miezi miwili baadae yaani Mei 2020 Clubhouse ilikua na watumiaji 1500 hadi Desemba 2020 mtandao huo ulikuwa na watumiaji 600,000. Hadi kufikia Januari 2021 mtandao huo ulikuwa na watumiaji zaidi ya milioni 10 kwa wiki.

Kuanzia mwaka jana mtandao huo ulipoanzishwa hadi Aprili mwaka huu mtandao huo ulikuwa ukipatikana kwa watumiaji wa simu zenye uwezo wa IOS hadi mwezi Mei mwaka huu (2021) mtandao huu umeanza kupatikana kwa watumiaji wa Android. Ni bahati yangu pia kuwa miongoni mwa watumiaji wa Android walioanza kutumia mtandao huo mara moja ulipopatikana kwenye simu za Android.

CLUBHOUSE NI NINI?


 

Inawezekana mpaka sasa  unajiuliza mtandao wa clubhouse upoje na je ni kama ilivyo mingine kama vile whatsapp, Instagram, facebook, tiktok na mingineyo.

Clubhouse yenyewe ipo tofauti kidogo. Mtandao huu unatumia njia ya sauti pekee ambayo watumiaji huweza kujiunga kwenye club mbalimbali ili kusikiliza mada ambazo zinakuwa kwenye club tofauti tofauti.

Na uzuri ni kwamba mnapomaliza mazungumzo yenu yanafutika hapo hapo.

Fikiria leo umeingia kwenye chat room unapenda muziki na unasikiliz Daimond au Alikiba wakizungumzia namna wanavyotengeneza muziki mzuri.

Au waza wewe ni mwanasoka na unaingia kwenye chat unakutana na Samatta akizungumzia mada ya mchezaji bora anakuwaje.

Au tuseme wewe ni mjasiriamali, unaingia unakuta Moh Dewji au Dangote wakieleza mbinu mbalimbali za kufanikiwa kwenye ujasiriamali.

Au unapenda mambo ya siasa, utamsikiliza Zitto Kabwe na Januari Makamba wakiwa kwenye jukwaa moja na wakichangia hoja mbalimbali.

Hii ndiyo clubhouse itakayokuwezesha si tu kukukutanisha na watu lakini pia kujifunza mambo mbalimbali kwa gharama nafuu ambazo tumezoea watu wakiwa wanatumia gharama kubwa kufika kwenye semina na warsha mbalimbali.

Wakati naandika makala hii nipo kwenye jukwaa la wanamuziki ambapo watu wanaimba na watu wengine wanawapa nini cha kuongeza. Mtandao kama huu unaweza kukutanisha na watu ambao wanaweza kuwekeza kwako, kama usipojificha. Ama kweli sasa dunia ni kama kijiji.

Hata wachungaji pia wanaweza kuutumia mtandao huu kulitangaza neno la Mungu. Hii ndiyo Clubhouse.

Ili kupata kujiunga na mtandao huu lazima mtu aliyejiunga na mtandao huu akuweke ndo unaanza kupatikana kwenye mtandao. Ukifungua jina la mtandao wa mtu fulani utaona aliwekwa na mtu fulani ambaye alitangulia kuwa kwenye mtandao hupo.

Mfano mimi Edius Katamugora niliwekwa na Jacob Mushi.

Kama unataka kujiunga na mtandao huu unaokua kwa kasi sana. Pakua App yake inayopatikana bure playstore au Apple store kisha muombe mtu akuunge.

Naweza kukupa huduma hiyo pia, sevu namba yangu 0764145476 (Edius Katamugora) kisha niambie nisevu yako na ukishaipakua App utajisajili kisha italeta ombi la wewe kutaka kujiunga.

Jiunge na ulimwengu huu mpya wa teknolojia inayokuwezesha kujifunza toka kwa magwiji.

Tafadhali, usomapo ujumbe huu, share na kwa wenzako pia. Sharing is caring.

Imeandaliwa Na

Edius Katamugora

0764145476 

Hii ni blogu rasmi ya Edius Katamugora, hapa utajifunza maendeleo binafsi, utapata makala mbalimbali zinazohusu biashara, elimu, hamasa na maisha kwa ujumla. Karibu sana katika blogu hii.

1 comments:

Unknown said...

Kazi nzuri...Asante