Headlines
Loading...

Thursday 13 May 2021

UNAINZAJE SIKU YAKO?

                                     

Kila asubuhi ni namna mpya ya kumshukuru Mungu kutupa uwezo na pumzi ya kuendelea kuishi.

Hii ni fursa wanayoipata wachache na wala si haki. Wakati unashtuka Leo usingizini kuna mtu alikua anavuta pumzi yake ya mwisho.

...Hilo tu linapaswa kukupa sababu ya kumshukuru Mungu wewe kuendelea kuishi. Bado unayo mengi ya kuifanyia dunia.

Hakuna aliyekuja duniani kuzurura wala kusindikiza wengine, lakini muda mwingine tunaishi kama tumekuja kusindikiza wengine.

Kuna Yule mtu anasema, "Kuna wengine wanaishi, sisi tunaishia." 

Nikuombe kitu kimoja usikubali kuishia.

Huo ni utangulizi Tu wala sikupanga kuongelea Jambo hilo lakini nimeona tu niwakumbushe.

Nirudi kwenye swali langu, unainzaje siku yako?

Baada ya kuamka kitandani na kumshukuru Mungu nini hufuata?

Njia njema na tabia tabia unayopaswa kuifanya ni kuianza siku yako kwa kufanya mazoezi ya mwili.

Amka kitandani, nenda barabarani anza kufanya mazoezi. Kimbia fanya jogging, na mengineyo.

Tabia hii inabidi uifanye kabla dunia haijaamka. Wakati wengine wamelala wewe tayari umeamka.

Mazoezi ni afya, jali afya yako. Usisubiri uwe na magonjwa, sijui presha mara kisukari ndo uanze kufanya mazoezi.

Ukitumia nusu  saa kwenda geuka rudi nyumbani utakua umetumia karibia lisaa.

Mazoezi ya asubuhi si kwamba yanakusaidia kiafya tu hata utendaji.

Namna yako ya kufikiri huwa ya tofauti. Yaani unaiona dunia Kwa jicho  la tatu ama upeo tofauti.

Mazoezi yatakufanya uwe na maamuzi yaliyo nyooka.

Mazoezi ni uraibu(addiction) unaotakiwa kuujenga kwasababu si uraibu hasi bali ni chanya.

Uraibu chanya ni  ule unaoboresha maisha yako. Uraibu hasi ni ule unaoharibu ubora wa maisha yako kama vile uvutaji sigara.

Kinachotokea unapofanya mazoezi ya asubuhi kama kukimbia barabarani asubuhi ni kwamba mnamo Dakika ya arobaini ubongo wako unazalisha kemikali zinazojulikana kitaalamu kama "kemikali za kusavaivu(survival chemicals). 

Majina ya kemikali hizi kwa nianvyojua ni beta endorphins na nerophinphrine. Hizi kemikali huufanya mwili ujisikie poa, sana.

Wakati wengine wanaamka wakiwa wamekereka wewe unainza siku yako kwa uchangamfu.

"Maisha huanza kila asubuhi." (Joel Osteen)


Hii ni blogu rasmi ya Edius Katamugora, hapa utajifunza maendeleo binafsi, utapata makala mbalimbali zinazohusu biashara, elimu, hamasa na maisha kwa ujumla. Karibu sana katika blogu hii.

0 comments: