Tuesday 11 May 2021

YAH: KUWA NA MAHUSIANO YANAYOELEWEKA



Mojawapo ya kitu kitakacho kufikisha mbali ni kuwa na mahusiano yanayoeleweka.

Sio rahisi kukuta mtu ana wake wengi ukakuta ana maisha yaliyonyooka, tazama hata vijana ambao unakuta kila uchao anamahusiano na mtu mpya, akili zao ni  kupata pesa za kula na kuvaa, full stop.

Hawawezi kingine, hawana malengo hawana mipango na hakuna kitu chochote cha maana wanachofanya.

Ukiwa na mahusiano mengi lazima muda wako ufie huko, utaongea na huyu ukimaliza utampigia huyu. Au ukimaliza kuonana na huyu utaenda kwa kwa yule matokeo yake ni kupoteza muda Tu.

Kwenye Kitabu cha Matatizo si tatizo (Matatizo ni Daraja) Fr. Faustin Kamugisha ametoa stori ya HENRY FORD.

Henry Ford ni mwanzilshi wa kampuni ya kutengeneza magari aina ya Ford.

Akiwa anatimiza Jubilei ya miaka 25 ya ndoa yake, MC alimuuliza aseme nini Siri ya mafanikio ya ndoa yake.

Alijibu, "Siri ni ile ile ninayo tumia kwenye magari, sijawahi badili modeli ya gari."

Wewe unabadili modeli kila siku. Unakutana na mdada mwaka mmoja tu amekuwa kwenye mahusiano na watu 7 tofauti unajiuliza maswali hadi unakosa jibu.

Wakaka ndo usiseme, Leo anapost huyu kesho Yule, yaani vurugu mechi.

Niliandika kwenye kitabu changu cha PUMBA ZA EDIUS "Hakuna fomula inayosema kwamba ukitoka kwenye uhusiano mmoja unganisha na kuanza mwingine. Muda mwingine unahitaji kuwa peke yako ujitafakari na kugundua ulifeli wapi. Jipe muda. Sio lazima kila wakati uwe kwenye uhusiano, muda mwingine unahitaji kuwa na uhusiano na wewe mwenyewe."

Kabla ya kuandika kitabu chake cha THINK AND GROW RICH Napoleon Hill aliwahoji matajiri Zaidi ya 500 ili kupata majibu ya nini kiliwafanya wawe matajiri kuwa na mahusiano yanayoeleweka lilikuwa jibu mojawapo.

Usichukulie poa mahusiano, Yana mchango mkubwa kwenye kufanikiwa au kutofanikiwa kwako.

Imeandaliwa Na
Edius Katamugora
ekatamugora@gmail.com
0758594893 (WhatsApp)

Hii ni blogu rasmi ya Edius Katamugora, hapa utajifunza maendeleo binafsi, utapata makala mbalimbali zinazohusu biashara, elimu, hamasa na maisha kwa ujumla. Karibu sana katika blogu hii.

0 comments: