Friday 31 March 2017

Ukiwa Na Imani Unaweza Kuhamisha Milima




Habari mpendwa msomaji wa Bideism Blog. Ni matumaini yangu kwamba umeamka salama na unaendelea vizuri na majukumu yako. Nikukumbushe kwamba leo ni siku yako muhimu sana kwako usikubali ipotee. One day can make you grow.
''Amini, nawaambia mkiwa na imani, msipokuwa na shaka, mtafanya si hilo la mtini tu, lakini hata mkiuambia mlima huu, Ng'oka ukatupwe baharini, litatendeka." (Mathayo 21:21).
   Amini na amini kwamba unaweza kuamisha mlima na unaweza kwa asilimia mia. Watu wengi hawaamini kwamba wanaweza kuhamisha milima na wanajikuta hawafanyi hivyo.
Katika dunia hii ya leo kuna watu wengi waliohamisha milima na kuitupa baharini. Hawa ni watu wenye imani. Na katika sheria za asili zilizokuwepo toka miaka elfu kabla ya Kristu ni sheria ya uvutano ( law of attraction) kwenye sheria hii iliyojigawa Mara tatu, imani imesimama kama nguzo ya tatu.
Kuamini kuna nguvu kubwa katika maisha ya mwanadamu na sio nguvu tu ata miujiza.
Imani inafanya kazi namna hii;
Ukiwa na imani kwamba "nipo chanya na naweza" mtizamo, unatoa msukumo wa nguvu na ujuzi unaofanya jambo Fulani, ukiwa na imani kwamba " naweza kufanya jambo Fulani" namna ya kufanya jambo hilo inajileta yenyewe.
Zamani watu waliamini barua ni nusu ya kuonana. Lakini Alexander Graham Bell alikuwa na imani zaidi akaisaidia dunia kugundua simu. Hatutumii tena barua kwa kiasi kikubwa.
Watu hawakuamini kwamba mtu anaweza kuelea angani. Wright Brothers kuziilisha jambo hilo wakaamua kutengeneza ndege. Leo hii tunaelea angani.
Isingekuwa imani nadhani hadi leo hii tungekuwa tunatumia vibatari na chemli. Bwana Edson Thomas ilimpasa afanye majaribio zaidi ya elfu moja ndipo alipogundua taa inayotumia umeme, maarufu kama balbu ( light bulb). Ni imani iliyoje!.
Henry Ford alikua na imani na picha ya gari lenye kutumia silinda nane. Mainjia wake walimwambia zaidi ya Mara 5 kwamba haiwezekani. Yeye aliwaambia linawezekana. Hatimaye aliwalazimisha hadi wakapata uwezo wa kutengeneza gari hilo. Leo tunaona V8 zinanesa tu barabarani. Lakini mwanzoni hata mainjinia walijua gari hilo haliwezi kutengenezwa. Ni kutokana na imani ya Ford tu jambo hili limewezekana.
     Chrispher Columbus aliamini kwamba kuna kuna dunia mpya ( new world) ..Ndiyo dunia tunayoishi leo hii.
  Mwaka 1952, Bwana Edmund Hillary alishindwa kupanda mlima Everest wenye futi 29,000 kutoka usawa wa bahari, baada ya kushindwa alichukua picha ya mlima huu na kusema maneno haya "Mlima Everest, ulinipiga siku ya kwanza, lakini nitakupiga siku zinazofuata, kwakuwa umekua kufikia ukomo, lakini Mimi naendelea kukua."
 
Kwa imani hii hatimaye tarehe 29, mei mwaka 1953 aliweza kuwa mtu wa kwanza duniani kupanda mlima Everest. Kuna nguvu kubwa katika imani na kile unachokiamini. Ukisoma pia historia ya Abraham Lincoln utagundua alikuwa na imani kubwa. Ni mtu aliyekosa nafasi nyingi za uongozi lakini akuchoka kugombea na hatimaye alipata kuwa raisi wa Marekani.
Watu wengi waliofanikiwa wanaongozwa na imani, kila siku wanang'oa milima na kuitupa baharini. Hata wanasayansi pia wanaongozwa na imani katika kufanya majaribio yao ndio maana wanaendelea hawaachi kwani wanaamini kuna kitu watakigundua.
" Amini nawaambia mkiwa na imani, msipokuwa na shaka, mtafanya sio hilo la mtini tu, lakini hata mkiuambia mlima huu, Ng'oka ukajitupe baharini, litatendeka." Mathayo 21:21
Ask-belive-receive (Law of attraction).
Ni Mimi rafiki na ndugu yako.
Edius Bide Katamugora
Tuwasiliane;
0764145476
0625951842 (Whatsapp)
Email; ekatamugora@gmail.com
Usisahau kuunganisha email yako hapo chini ya Makala hii.
"See you at the top."

Wednesday 29 March 2017

Mawazo Yanakuwa Vitu



Habari mpendwa msomaji wa Bideism Blog. Ni matumaini yangu kwamba wewe rafiki yangu umeamka salama na umejiweka tayari kuhakikisha unanufaika na siku ya leo. Nidhidi tu kukumbusha kwamba leo ni siku muhimu usikubali ipotee hivi hivi. One day can make you grow
Karibu katika Makala ya leo inayosema " Mawazo huwa vitu". Thoughts become things. Hii ni ufupisho wa sheria ya asili kabisa iliyokuwepo toka enzi za mababu hadi leo hii. Toka kizazi cha kina Plato,Socrates, Edson, Ford,Roosevelt, hadi kina Steve Jobs, Bill Gates kutaja wachache. Sheria hii inajulikana kama sheria ya uvutano( The law of Attraction). Inayosema vitu vinavyofanana uvutana vyenyewe kwa vyenyewe ( Like attracts like).
Kwa undani sheria hii inazungumzia kwamba jinsi ulivyo leo ni kutokana na mawazo yako ya siku za nyuma. Ndiyo maana nikaipa Makala hii " Mawazo yanakuwa vitu". Ubongo na akili zetu ni kama sumaku kile tunachokiweka na kukifikiria Mara nyingi Mara kwa Mara ndicho kinachotokea kwenye maisha yetu.
Utabisha ya kwamba nimeandika uongo lakini ukweli utabaki kuwa hivyo. Ulivyo wewe leo ni kutokana na mawazo yako ya siku za nyuma. Mwandishi wa Kitabu cha " How to live 365 days" Dr. Sandler aliyefariki dunia mwaka 1957, anasema kati ya wagonjwa 4 waliolazwa kwenye vitanda vya hospitali watatu hawaumwi. Wanakuwa wanawaza kuumwa na hatimaye wanajikuta katika hali hiyo. Hii imewatokea wengi pale unsjihisi kuumwa ukienda hospitali kupima haoni lolote kwa maana kwamba huumwi. Ni kutokana na sheria hii ya uvutano. Unavyofikiri ndivyo unavyokuwa.
Kumbe mawazo yetu yanachangia kikubwa katika maisha yetu. Picha unayoiona leo kwenye maisha yako kuhusu kesho ndo hile hile itakayotokea. "Uzuri ni kwamba sheria hii haindani kabisa na muda inatupa muda wa kubadilisha picha zetu tunazoziona kila siku la sivyo maisha yangelikuwa magumu" anasema Lisa Nichols mwandishi wa Vitabu na muhamasishaji.
Jambo la msingi tunalopaswa kujifunza hapa kutokana na sheria hii ni kwamba inabidi tujenge picha chanya katika maisha yetu. Jinsi unavyojijengea picha chanya ndivyo akili yako inavyokusukuma kufanyia kazi picha unayoiona. Na jinsi unavyojijengea picha hasi ndivyo akili yako inavyokusukuma kuelekea mambo hasi. Ndiyo maana kuna watu walikuwa matajiri baadae wakafirisika na baadaye wakarudi kwenye utajiri wao wa zamani kwa sababu ya kutumia sheria hii. Raisi wa Marekani Bw. Trump ni mfano wa watumiaji wazuri wa kanuni hii aliwahi kufirisika miaka ya mwanzoni lakini baadae alirudisha utajiri wake.
Nawewe rafiki yangu nakusihi leo anza kutumia kanuni hii itakupa matokeo makubwa na naamini utanipenda. Kama leo umeamka na kusema "hii ni siku mbaya kwangu" badilisha sasa hivi na kusema " Leo ni siku nzuri sana kwangu, nitafanya makubwa". Fanya hivyo utaona maajabu makubwa. Kumbuka kama huna furaha ni kwasababu tu umekuwa ukiwaza mambo yasiyokuletea furaha. Na ujinga wa kuwaza mambo hasi ni kwamba ukiwaza jambo hasi moja mawazo mengine lukiki hasi yanajizakisha ( When you think of one negative thoughts other more negative thoughts do generate).
Ni Mimi rafiki na ndugu yako
Edius Bide Katamugora
Life Coach/Author/Motivation speaker.
0764145476
0625951842 ( Whatsapp)
Email; ekatamugora@gmail.com
Usisahau kutuma email yako hapa chini ili izipate Makala zangu moja kwa moja au tuma neno "Subscribe" kwenye namba ya whatsapp niliyoandika hapo juu niwe nakutumia Makala hizi.

Tuesday 14 March 2017

Thursday 9 March 2017

SPIRITUAL DEVELOPMENT
Blessed are those who trust in the Lord...
They are like trees planted along a riverbank, with roots that reach deep into the water. Such trees are not bothered by the heat or worried by long months of drought. Theur leaves stay green.and they go right on producing delicious fruit.
            Jeremiah 17;7-8 (NLT)