Monday 19 December 2016



                                          UJACHELEWA
Habari mpendwa msomaji wa Bideism blog. Ni matumaini yangu kwamba umeamka salama siku ya leo na unaendelea kupambana kuelekea mafanikio.
 
Je ni mara ngapi umeshindwa  kufanya kitu Fulani na ukahisi umechelewa?. Umefeli mtihani na ukuweza kuendelea na masomo, umeanzisha biashara au mradi Fulani haujafanikiwa, umeachwa na mpenzi wako au umetupwa na ndugu jamaa na marafiki, umehachishwa kazi au umefukuzwa kazi. Je unahisi umechelewa kimaisha?. Leo ninayofuraha kubwa kukwambia ujachelewa.

‘’ Anguka mara saba simama mara nane’’ ni msemo wa Kijapani. Kumbe tunapoangua tusibaki palepale chini hatuna budi kusimama na kusonga mbele. Kama umefukuzwa kazi uenda ndio umefunguliwa milango yakupata kazi nzuri zaidi yenye kukupa furaha na wakati mwingine yenye kipato zaidi. Kama umeshindwa mtihani uenda huu ndio muda wako muafaka wa kufanya maajabu mapya katika historia ya elimu yako. Kama  umeachwa na mpenzi wako uenda ndio muda muafaka wa kumpata mtu sahii wa mahusiano yako. Kumbe bado ujachelewa. ‘’ Mabadiliko makubwa yako mikononi mwako’’ alisema raisi wa zamani wa Marekani Bwana John F. Kenedy.  Ivo basi tusikate tamaa kwani kila kitu kipo ndani ya uwezo wetu. Jambo la msingi hapa ni kukaa chini na kutafakari kwa makini mambo yaliyosababisha tuanguke na kuyarekebisha kwani ‘’ Mtu ambaye anafanya makosa na hafanyi jitihada yoyote kuyarekebisha au kuyasahihisha  anakuwa anaendelea kufanya makosa ‘’ alisema Confucius. Usibaki tu kuwaza kama umechelewa kwani msongo wa mawazo ni sanaa ya kutengeneza matatizo ambayo hata kabala hayakuwepo. Unapocheleweshwa uenda ndipo unapolenga mahala sahihi katika maisha yako kwani ili mshale ufikie lengo lazima uvutwe kurudi nyuma. Kumbe kurudi nyuma si kuchelewa bali kulenga mahali sahii.

Bwana Brian Acton mwanzilishi wa mtandao wa kijamii maarufu kama WHATSAPP mwaka 2009 alikataliwa kufanya kazi na kampuni ya YAHOO kama mwandisi wa kampuni hiyo. Mwaka huo huo pia alikataliwa kuajiriwa na kampuni ya FACEBOOK. Alikwenda na kubuni WHATSAPP mwaka huo huo wa 2009. Mwaka 2014 kampuni ya FACEBOOK iliununua mtandao huo wa WHATSAPP kwa dola za Kimarekani zipatazo bilioni  2.8. leo hii ni bilionea. Huyu ni mfano wa watu ambao labda tungesema wamechelewa lakini hakuchoka kupigana hatimaye akafikia ziadi hata ya ndoto zake. 
’ Dunia inapokusukuma kwenye magoti inakupa wakati muafaka wa kusali’’ alisema Rum. 

  Tufahamu kwamba tunaitaji kuweka juhudi kubwa ili kuyafikia malengo yetu. Tuondoe dhana vichwani mwetu kwamba tumepotea njia, hata Roma haikujengwa kwa siku moja. ‘’ Mlango mmoja unapofungwa, mwingine unafunguliwa , lakini wakati mwingi tunayaacha macho yetu yakiangalia kwa majuto mlango uliofungwa kiasi cha kutoweza kuona mlango mpya uliofunguliwa kwa ajili yetu ‘’ alisema  Alexander Graham Bell.

Mwandishi wa kitabu cha RICH DAD, POOR DAD Bwana Robert Kiyosaki anasema kwambwa ‘’ Sijawahi kuona mtoto mdogo anayejifunza kutembea na hasianguke, sijawahi kuona mtu anayejifunza kuendesha  baiskeli ambaye hajawahi kuanguka, sijawahi kukutana na mtu ambaye aliwahi kupenda na hajawahi kuumizwa na sijawahi ona mtu tajiri ambaye ajawahi poteza pesa’’.  Raisi wa Marekani TRUMP anaongezea na kusema ‘’ ili ufanikiwe lazima uanguke mara nyingi na katika kuanguka utajifunza mengi’’.
Hivyo basi ndugu yangu na rafiki yangu usihisi umechelewa katika kile ulichozamilia ili kufikia malengo na ndoto zako. Weka mbinu mpya, mikakati mipya itakayokuwezesha kufikia malengo yako. Badili mtazamo wako, kuwa chanya, epuka watu watakaokwambia hutoweza kwani wao sio wewe. Wakati wako ndio leo wakati wako ndio sasa.

Siku moja bwana mmoja alikua akienda mjini kufanya mahojihano ya kazi, hivo aliamka asubuhi na mapema kwani alikua akiishi mbali kidogo na mjini. Alifika kwenye kituo cha basi na kupanda kwenye gari wa kwanza. Baadae kidogo watu wengine walianza pia kupanda gari. Bwana huyo alitoka kwenye gari na kwenda dukani kununua vocha na maji ya kunywa na aliporudi alikuta konda amekwisha uza siti yake. Aliogombeza sana konda na akifikiri kua ulikuwa ndio mwanzo wa kuipoteza kazi ile muhimu katika maisha yake. Bwana uyo aliamu kwenda kupanda gari lingine akiwa ametingwa na mawazo mengi kichwani, kwani gari alilopanda lilimuacha na kutangulia. Baada ya muda kidogo gari alilopanda likawa limejaa na hivyo kuanza safari. Saa moja baada ya kuanza safari njiani walikutana na ajari mbaya sana iliyohusisha basi na roli ambapo kila mtu aliyekuwa kwenye basi alifariki dunia. Kumbe basi lililomuacha ndilo lile lililopata ile ajari mbaya. Kumbe kuna wakati tunaweza ng’ang’ania kitu Fulani wakati Mungu amekwisha tupangia kitu Fulani chema kama mwelekeo wetu kabla hatujazaliwa alikwisha panga maisha yetu yatakuwa ya namna gani. Kuna wakati tunajishikiza kwenye mambo yaliyopita pasipokujua tunapoteza Baraka mpya. Mungu anawatoa watu kutoka katika matatizo na kuwapeleka katika nchi ya ahadi. Yosefu alidhani ulikuwa mwisho wake wa maisha alipouzwa kama mtumwa lakini kumbe ulikuwa ndio mwanzo mzuri wa kwenda kuonyesha vipawa vyake vya uongozi na hatimaye kuwa waziri mkuu katika nchi ya ugenini Misri. Kuna mambo mengine yanatokea katika maisha yetu ambayo yako nje ya uwezo wetu.Kila unapoanguka kwa namna moja au nyingine unapata fursa ya kujifunza kitu kipya, usikate tama. Ndoto yako ni kubwa kwa kadri unavyoweza kuota na kupigana kufikia ndoto yako. Kuna muda unaweza kuona kama ndoto yako huioni, haina maana kwamba huioni ni sababu kwamba haitakuja, unapokwenda kwenye kituo cha magari unasubiri magari kwasababu yatakuja na huondoki eti kisa gari limechelewa kufika. Kama huoni matumaini katika maisha yako haimaanishi kwamba hayapo. BADO HUJACHELEWA.

Ni mimi rafiki na ndugu yenu.
Edius Bide Katamugora.

Tuwasiliane;
0764145476.
Whatsapp; 0625951842  (tuma neno SUBSCRIBE niwe nakutumia makala zangu moja kwa moja whatsapp)
email; ekatamugora@gmail.com

Endelea kusoma makala nyingine nzuri kama hizi hapa. Asante

'' See you at the top'' 

Hii ni blogu rasmi ya Edius Katamugora, hapa utajifunza maendeleo binafsi, utapata makala mbalimbali zinazohusu biashara, elimu, hamasa na maisha kwa ujumla. Karibu sana katika blogu hii.

0 comments: